Tuesday 29 April 2008

Wasomi waukosoa Muungano

Wasomi waukosoa Muungano
na Mwanne Mashugu, Zanzibar
SIKU moja baada ya kupita kwa sherehe za miaka 44 ya Muungano, wanafunzi kadhaa wa vyuo vikuu visiwani hapa, wamesema mabadiliko kuhusu hadhi ya Rais wa Zanzibar katika Serikali ya Muungano, ni kasoro kubwa inayopaswa kurekebishwa haraka.
Kutokana na kasoro hiyo, wanafunzi hao walishauri Serikali ya Muungano kurejesha haraka utaratibu wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Walisema marekebisho ya sheria yaliyomuondolea hadhi Rais wa Zanzibar kushika wadhifa huo, umeishushia hadhi yake Zanzibar katika nyanya ya kimataifa.
Wanafunzi hao walisema hayo walipokuwa katika kongamano kuadhimisha miaka 44 ya Muungano wa Tanzania.
Hadhi ya Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Muungano iliondolewa kupitia mabadiliko ya 11 ya Katiba ya Muungano.
“Rais wa Zanzibar mamlaka yake yameondoka katika nyanja za kimataifa na uraia wetu umepotea kwa vile hata misaada inaishia Tanzania Bara,” alisema Khamis Issa Mohammed wa Chuo cha Elimu Chukwani.
Katika kongamano hilo lililoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, Haji Habib Kombo alisema kwamba hivi sasa Rais wa Zanzibar analazimika kuingia katika Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano kama waziri asiyekuwa na wizara maalum, jambo ambalo halileti picha nzuri.
Aidha, mwanafunzi huyo alibainisha kuwa hata mfumo uliopo, hauonyeshi kinagaubaga mamlaka aliyonayo makamu wa rais.
Akifafanua, alisema kuwa licha ya taratibu kueleza vinginevyo, lakini hali halisi inaonyesha kuwa mamlaka ya utendaji ya Waziri Mkuu ni makubwa kuliko ya Makamu wa Rais, suala ambalo linahitaji kuangaliwa upya, ili kurejesha hadhi ya Makamu wa Rais.
“Bila ya Zanzibar hakuna Tanzania, na bila ya Afro Shiraz Party hakuna CCM… marekebisho ya katiba yafanyike kumpa hadhi Rais wa Zanzibar,” alisisitiza.
Alieleza kuwa mfumo huo mbaya wa Muungano, hauathiri katika masuala ya utawala pekee, bali pia katika nyanja nyingine.
Alisema kuwa kutokana na mfumo huo, Zanzibar imekuwa ikiathirika kiuchumi na kutoa mfano kuwa pamoja na elimu ya juu kuwa suala la Muungano, hakuna chuo kikuu hata kimoja kilichojengwa na Serikali ya Muungano visiwani Zanzibar.
Kombo alisema kwamba Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kinapaswa kupokea ruzuku kutoka Serikali ya Muungano, badala ya kuendeshwa kwa gharama za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar peke yake kama ilivyo sasa.
Issa Kheri wa Chuo cha Elimu Chukwani alisema kwamba kero za Muungano zinachelewa kupatiwa ufumbuzi kutokana na viongozi kutozipa umuhimu.
Alisema kwamba zipo ripoti nyingi zilizokusanywa juu ya Muungano, ikiwemo ile ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, lakini inashangaza kuwa hadi sasa mapendekezo yake hayajatekelezwa.
Alisema kwamba iwapo ripoti ya Jaji Kisanga na Francis Nyalali zingefanyiwa kazi, hivi sasa kero nyingi za Muungano zingekuwa zimeshamalizwa.
Alieleza kuwa badala ya kutekeleaa mapendekezo ya Tume ya Jaji Kisanga, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, alitumia muda mwingi kumshambulia jaji huyo, kwa kutoa ripoti hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inawakilisha maoni ya wananchi.
“Tume nyingi zimeundwa ikiwemo ile ya Jaji Kisanga, ikafanya kazi nzuri tu, lakini Rais mstaafu Mkapa akamshambulia kutokana na maoni yaliyopendekezwa na wananchi,” alisema.
Alieleza kwamba hakuna njia itakayosaidia kuwa na Muungano bora zaidi ya wananchi kushirikishwa na kuamua kwa kupitia utaratibu wa kura ya maoni.
Alisema kwamba hivi sasa historia ya Tanganyika ipo hatarini kupotea, kwa vile baadhi ya Watanzania wanaoishi Zanzibar wanapoambiwa wanatoka Tanganyika, wanahisi kama wanatukanwa.
Naye Omar Suleiman, alisema kwamba kero za Muungano haziwezi kutatuliwa kwa makongamano, bali kwa wananchi wa Zanzibar kujenga umoja, ili kuhakikisha matatizo yote ya Muungano yanatatuliwa kwa muda muafaka.
Alisema kwamba Zanzibar inashindwa kusonga mbele kutokana na tabia iliyojitokeza ya majungu na kuendeleza tofauti za Unguja na Pemba na hivyo kuzorotesha maendeleo ya wananchi.
“Jambo la msingi sisi Wazanzibari tuwe na msimamo, tuache tabia ya fitina na ubaguzi kwa misingi ya Upemba na Uunguja, ili tuweze kusonga mbele kutatua matatizo ya Muungano,” alisema.
Alisema Zanzibar hivi sasa ni nchi kamili yenye utawala wake, lakini rais wake hana nguvu nje ya Zanzibar.
Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Said Mzee, alisema kwamba Zanzibar inarudi nyuma kutokana na wasomi wake kuwa waoga na kushindwa kujitokeza kudai mambo ya msingi ya nchi yao.
Alisema kwamba njia nyingi za kiuchumi Zanzibar zimevurugwa na mfumo mbaya wa Muungano, lakini wasomi wengi wamekaa kimya licha ya wao na jamii kuguswa na masuala hayo.
Makamu mwenyekiti huyo alisema vikao vya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi havitasaida kutatua kero za Muungano. Alishauri kuwa watu wengi zaidi washirikishwe katika kujadili masuala ya Muungano, kwa vile mambo hayo yanagusa taifa na si CCM au serikali pekee.
Aidha, alisema kuwa udhaifu wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika utekelezaji majukumu yao, umechangia Zanzibar kukabiliwa na matatizo mengi ya kiuchumi yakiwemo yaliyo nje ya Muungano.
“Wawakilishi wetu hawana elimu ya kutosha katika kujadili mipango ya maendeleo na kiuchumi, ndiyo maana Baraza la Wawakilishi limedorora, hawa ni wazee wetu tunawaheshimu, lakini ukweli wanaburuzwa na serikali,” alisema.
Alieleza kwamba umefika wakati wajumbe wa baraza hilo kufuata nyayo za Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe, aliyekubali kujitolea kutetea maslahi ya wananchi na taifa.

Wasomi waukosoa Muungano

na Mwanne Mashugu, ZanzibarSIKU moja baada ya kupita kwa sherehe za miaka 44 ya Muungano, wanafunzi kadhaa wa vyuo vikuu visiwani hapa, wamesema mabadiliko kuhusu hadhi ya Rais wa Zanzibar katika Serikali ya Muungano, ni kasoro kubwa inayopaswa kurekebishwa haraka. Kutokana na kasoro hiyo, wanafunzi hao walishauri Serikali ya Muungano kurejesha haraka utaratibu wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano. Walisema marekebisho ya sheria yaliyomuondolea hadhi Rais wa Zanzibar kushika wadhifa huo, umeishushia hadhi yake Zanzibar katika nyanya ya kimataifa. Wanafunzi hao walisema hayo walipokuwa katika kongamano kuadhimisha miaka 44 ya Muungano wa Tanzania. Hadhi ya Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Muungano iliondolewa kupitia mabadiliko ya 11 ya Katiba ya Muungano. “Rais wa Zanzibar mamlaka yake yameondoka katika nyanja za kimataifa na uraia wetu umepotea kwa vile hata misaada inaishia Tanzania Bara,” alisema Khamis Issa Mohammed wa Chuo cha Elimu Chukwani. Katika kongamano hilo lililoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, Haji Habib Kombo alisema kwamba hivi sasa Rais wa Zanzibar analazimika kuingia katika Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano kama waziri asiyekuwa na wizara maalum, jambo ambalo halileti picha nzuri. Aidha, mwanafunzi huyo alibainisha kuwa hata mfumo uliopo, hauonyeshi kinagaubaga mamlaka aliyonayo makamu wa rais. Akifafanua, alisema kuwa licha ya taratibu kueleza vinginevyo, lakini hali halisi inaonyesha kuwa mamlaka ya utendaji ya Waziri Mkuu ni makubwa kuliko ya Makamu wa Rais, suala ambalo linahitaji kuangaliwa upya, ili kurejesha hadhi ya Makamu wa Rais. “Bila ya Zanzibar hakuna Tanzania, na bila ya Afro Shiraz Party hakuna CCM… marekebisho ya katiba yafanyike kumpa hadhi Rais wa Zanzibar,” alisisitiza. Alieleza kuwa mfumo huo mbaya wa Muungano, hauathiri katika masuala ya utawala pekee, bali pia katika nyanja nyingine. Alisema kuwa kutokana na mfumo huo, Zanzibar imekuwa ikiathirika kiuchumi na kutoa mfano kuwa pamoja na elimu ya juu kuwa suala la Muungano, hakuna chuo kikuu hata kimoja kilichojengwa na Serikali ya Muungano visiwani Zanzibar. Kombo alisema kwamba Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kinapaswa kupokea ruzuku kutoka Serikali ya Muungano, badala ya kuendeshwa kwa gharama za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar peke yake kama ilivyo sasa. Issa Kheri wa Chuo cha Elimu Chukwani alisema kwamba kero za Muungano zinachelewa kupatiwa ufumbuzi kutokana na viongozi kutozipa umuhimu. Alisema kwamba zipo ripoti nyingi zilizokusanywa juu ya Muungano, ikiwemo ile ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, lakini inashangaza kuwa hadi sasa mapendekezo yake hayajatekelezwa. Alisema kwamba iwapo ripoti ya Jaji Kisanga na Francis Nyalali zingefanyiwa kazi, hivi sasa kero nyingi za Muungano zingekuwa zimeshamalizwa. Alieleza kuwa badala ya kutekeleaa mapendekezo ya Tume ya Jaji Kisanga, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, alitumia muda mwingi kumshambulia jaji huyo, kwa kutoa ripoti hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inawakilisha maoni ya wananchi. “Tume nyingi zimeundwa ikiwemo ile ya Jaji Kisanga, ikafanya kazi nzuri tu, lakini Rais mstaafu Mkapa akamshambulia kutokana na maoni yaliyopendekezwa na wananchi,” alisema. Alieleza kwamba hakuna njia itakayosaidia kuwa na Muungano bora zaidi ya wananchi kushirikishwa na kuamua kwa kupitia utaratibu wa kura ya maoni. Alisema kwamba hivi sasa historia ya Tanganyika ipo hatarini kupotea, kwa vile baadhi ya Watanzania wanaoishi Zanzibar wanapoambiwa wanatoka Tanganyika, wanahisi kama wanatukanwa. Naye Omar Suleiman, alisema kwamba kero za Muungano haziwezi kutatuliwa kwa makongamano, bali kwa wananchi wa Zanzibar kujenga umoja, ili kuhakikisha matatizo yote ya Muungano yanatatuliwa kwa muda muafaka. Alisema kwamba Zanzibar inashindwa kusonga mbele kutokana na tabia iliyojitokeza ya majungu na kuendeleza tofauti za Unguja na Pemba na hivyo kuzorotesha maendeleo ya wananchi. “Jambo la msingi sisi Wazanzibari tuwe na msimamo, tuache tabia ya fitina na ubaguzi kwa misingi ya Upemba na Uunguja, ili tuweze kusonga mbele kutatua matatizo ya Muungano,” alisema. Alisema Zanzibar hivi sasa ni nchi kamili yenye utawala wake, lakini rais wake hana nguvu nje ya Zanzibar. Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Said Mzee, alisema kwamba Zanzibar inarudi nyuma kutokana na wasomi wake kuwa waoga na kushindwa kujitokeza kudai mambo ya msingi ya nchi yao. Alisema kwamba njia nyingi za kiuchumi Zanzibar zimevurugwa na mfumo mbaya wa Muungano, lakini wasomi wengi wamekaa kimya licha ya wao na jamii kuguswa na masuala hayo. Makamu mwenyekiti huyo alisema vikao vya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi havitasaida kutatua kero za Muungano. Alishauri kuwa watu wengi zaidi washirikishwe katika kujadili masuala ya Muungano, kwa vile mambo hayo yanagusa taifa na si CCM au serikali pekee. Aidha, alisema kuwa udhaifu wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika utekelezaji majukumu yao, umechangia Zanzibar kukabiliwa na matatizo mengi ya kiuchumi yakiwemo yaliyo nje ya Muungano. “Wawakilishi wetu hawana elimu ya kutosha katika kujadili mipango ya maendeleo na kiuchumi, ndiyo maana Baraza la Wawakilishi limedorora, hawa ni wazee wetu tunawaheshimu, lakini ukweli wanaburuzwa na serikali,” alisema. Alieleza kwamba umefika wakati wajumbe wa baraza hilo kufuata nyayo za Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe, aliyekubali kujitolea kutetea maslahi ya wananchi na taifa.

Monday 28 April 2008

Wataka rais wa Z`bar awe Makamu wa Rais

Wataka rais wa Z`bar awe Makamu wa Rais2008-04-28 09:03:26 Na Mwinyi Sadallah, ZanzibarWanafunzi wa vyuo vikuu Zanzibar wamependekeza Rais wa visiwa hivyo ashike nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, ili awe na hadhi ya kimataifa anapokuwa nje ya nchi. Waliyasema hayo katika kongamano la vijana wa vyuo vikuu Zanzibar lililokwenda pamoja na maadhimisho ya miaka 44 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kongamano hilo liliandaliwa na Chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA). Akizungumza katika kongamano hilo, mmoja wa wanafunzi Bw. Haji Habib Kombo, wa Kitivo cha Sheria cha Chuo Kikuu cha Zanzibar, alisema, marekebisho ya 11 ya Tanzania iliyofuta wadhifa wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais yanapaswa kuangaliwa upya. Alisema mfumo uliokuwa ukitumika miaka ya mwanzo ya Muungano ulikuwa mzuri kwa vile ulimwezesha Rais wa Zanzibar kuwa na hadhi ya kimataifa anapokuwa nje ya nchi kama kiongozi wa Tanzania. Marekebisho ya katiba yaliyofuta Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano yalifanyika mwaka 1995 na kuweka utaratibu wa kuwa na mgombea mwenza. Alieleza kuwa mfumo wa uongozi katika serikali hivi sasa Waziri Mkuu anaonekana msaidizi wa Rais kuliko Makamu wa Rais. Aidha, alisema kitendo cha Rais wa Zanzibar kuingia katika Baraza la Mawaziri wa Muungano kama Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum hakileti tafsiri inayokubalika katika kuimarisha Muungano. Mwanachuo Yahya Alawi kutoka Chuo Kikuu cha Afya Mbweni alishauri kero za Muungano zitatuliwe haraka kwani zinachangia kuzorotesha maendeleo ya Zanzibar. Alisema utatuzi ukiendelea kuchelewesha utaleta athari kwa vizazi vijavyo kwa vile wananchi hawatakubali kuendelea na Muungano usio na faida kiuchumi. Alikumbusha kuwa wakati umefika hati ya Muungano kuonyeshwa hadharani ili kama kuna mapungufu yarekebishwe. ``Tuwe na Muungano unaokubalika baina ya pande zote, tunahofia vijana baadaye tutakuja kukamatana kutaka kujua faida na hasara za Muungano,`` alisema mwanafunzi huyo. Issa Kheri kutoka Chuo Kikuu cha Elimu Chukwani alisema ni jambo la kushangaza tume nyingi zimeundwa kushughulikia kero za Muungano, lakini utatuzi haujafanyika. Alisema iwapo mapendekezo ya ripoti ya Jaji Robert Kisanga yangetekelezwa kero nyingi zingekuwa zimetatuliwa. Aliongeza kuwa kuna matatizo mengi ya Muungano na kutaka wananchi kupewa fursa ya kuamua kwa njia ya kura ya maoni kuhusu aina ya Muungano wanaotaka. Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar, Bw. Said Mzee, alisema uwezo mdogo wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi umesababisha visiwa hivyo kuwa na matatizo makubwa. Alisema wawakilishi wanashindwa kukosoa serikali na kutetea kero za wananchi. Bw. Mzee alisema wajumbe wa baraza hilo wanaburuzwa na serikali kutokana kuwa na uwezo mdogo ikilinganishwa na wenzao wa Bunge la Muungano. SOURCE: Nipashe

Saturday 26 April 2008

Zanzibar's women plaster old city

Zanzibar's women plaster old city
By Daniel DickinsonBBC, Stone Town, Zanzibar
Years of neglect have left many buildings in Stone Town, the historic capital of the Indian Ocean island of Zanzibar, close to collapse - but now a team of women builders are trying to put that right.
The Indian Ocean island of Zanzibar is an iconic travel destination, known for white sandy beaches and its capital Stone Town, with its eclectic mix of Arab and African influences.
But what the travel brochures do not reveal is that Stone Town is crumbling.
However, a small army of women are trying to restore its labyrinthine alleys and carved wooden doors.
Among them is 31-year-old Asma Juma, one of six Zanzibari women who have been trained to plaster. She is part of a team restoring a dilapidated old spice house which will be reborn as a tourist hotel.
"When I started out it was difficult - you need to develop a technique, you need to be consistent and if you make a mistake, you need to admit to that mistake and start again," she says.
"Women are perfectionists, we like to get things right and that's why we're better at this job than men."
Women's work?
Asma has been doing this job for 18 months but she talks with the confidence of a master.
All the women have been taught by Vuai Mtumwa, who says that they all like the work because of their desire to renovate Stone Town.
"They work hard, they come every day," Mr Mtumwa says.

"They are working like men. Some work they can't do - they don't climb the scaffold."
Indeed, it is a physically tough place to work - with heavy lifting, precarious wooden scaffolding and the danger of falling rubble from work above.
And there are some who say women should not be working there at all.
'Women working on site in Zanzibar is not good," says Osumani Juma.
"If she has a husband she should stay home with the family. For men it is good to work here as it is difficult and dangerous.'
Despite the money that tourism brings, Zanzibar is still a poor island where unemployment is high.
"My family are happy that I'm doing this job," says Asha Mussa Ramadhani, another of the women plasterers.
"They think it's good work and I'm earning the same wage as the men. I think the men are annoyed because we are taking their jobs.
"I am the only one who is earning money in the family. It is god's will that I work here.
"I'm also happy because I'm helping to repair Zanzibar Stone Town and make it look nice again."
Beyond repair
Zanzibar Stone Town is a World Heritage site.
It is famous for its atmospheric, labyrinthine alleys, beautiful carved wooden doors, seafront palaces, and historic trading links with the Arab world.
But it is also a city that is slowly falling apart. I remember my first visit here several years ago, being shocked as I walked the back streets by the number of buildings in disrepair and the rubbish which I had to pick my way around.

A big problem, of course, is the lack of funding. On an island where most people earn less than a dollar a day, there is little money for restoration work.
Mohammed Mughery, from the Zanzibar Stone Town Heritage Society, fears for the future of Stone Town.
"There is little support we are getting from the government and other donors locally," he says.
"But the houses need to be repaired - most of the buildings haven't been repaired in 30-40 years. It is very strange.
"Most buildings are made of coral stone and lime mortar. So they need to be attended often. Just a small crack if left will become wider and will lead to the collapse of the building."
Although the heritage society is making its contribution by renovating the wall of an old trader's house, there are still dozens of other buildings which need urgent attention.
The women plasterers are ready to help out. They're just hoping that the funds are provided before Stone Town disintegrates beyond repair.