Friday 20 June 2008

Rostam Aziz na Vodacom-Tususie Ufisadi

Rostam Aziz yule mtanzania mwenye asili ya Kiiran aliyeko kwenye Orodha ya Mafisadi(List of Shame) anamiliki zaidi ya asilimia 30 ya hisa za Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kupitia kwa Kampuni yake ya Caspian ambayo pia inahusika na ufisadi katika kandarasi mbalimbali za ujenzi wa barabara, viwanja na hata migodoni. Je, wewe ni mtanzania unayechukia ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka?


Andika ujumbe huu na mtumie mwenzako mwenye Vodacom kwa SMS:

“Imegundulika, mtaji wa Vodacom sehemu kubwa ni fedha za ufisadi toka kwa Rostam Aziz. Tumia mtandao mwingine kuepuka kulipa fedha zako kuendeleza ufisadi. Ukijitoa kwenye ufisadi, unawapunguzia nguvu mafisadi. Sambaza Ujumbe”Au tuma ujumbe huu:“Afrika Kusini walivunja nguvu ya makuburu. Acha kuendelea kutunisha faida ya Fisadi Rostam Aziz. Achana na kampuni yake ya Vodacom. Tumia mtandao mwingine”.Au:“Je, wajua? Rostam Aziz anahisa nyingi Vodacom kwa fedha za ufisadi. Je, unataka kumwongezea fedha zaidi za kufanya ufisadi nchini? Okoa Taifa, jiunge na simu nyingine”.Au:“Kwanini utende dhambi kwa kuchangia katika ufisadi? Rostam Aziz ni mmoja wa wamiliki wa Vodacom. Tafakari, Chukua hatua”Au:“Ukipiga simu ana kutuma ujumbe kwa kutumia Vodacom unawaneemesha wamiliki mafisadi wakina Rostam Aziz, Noni na makuburu wa Afrika Kusini. Chagua ni lako”Au:“Vodacom, muondoe Rostam Aziz kabla watanzania hatujaucha mtandao wenu kwa kumilikiwa na watuhumiwa wa ufisadi. Tuma ujumbe huu kwenda 123, na mtumie na mwenzio”Au“Ama piga simu huduma kwa wateja namba 100; waulize Vodacom, je Rostam Aziz ni mmoja wa wamiliki? Wanasubiri nini mkutoa kwa ufisadi wake?
Habari za uhakikia kabisa ni kwamba Rostam Aziz ameanza kuhamishia mali zake nje ya nchi, sababu anahofia mambo yanavyokwenda serikalini kwa sasa. Kwa ushahidi tayari ameweka rehani hisa zake zote 35pc za Vodacom Afrika Kusini. Kabla ya kuhamishia hisa zake, alikua amenunua hisa za Planetel za mwenzake Peter Noni na mkewe, naye alifanya hivyo kuhofia mambo yanavyokwenda ofisini kwake BoT. Rostam alichukua hisa zote 35pc za Watanzania kupitia kampuni zake za Caspian na Mirambo. Chenge akiwa Waziri wa miundombinu alimsaidia kwa nguvu zake zote Rostam kufanikisha mkakati wake huo wa kuhamisha hisa zake nje kwa kisingizio cha kuweka rehani. Kuna watu serikalini walipinga (na wanaendelea kupinga) lakini jamaa aliwazidi kete kwa kusadiwa na Chenge na sasa inaelekea amefanikiwa kwa kiasi.

Sheria ya TCRA inasema kuhusu hisa za wazalendo kwamba wageni wasimiliki hisa zaidi ya 65% lakini Rostam Aziz aka RA anataka kuzipeleka nje zote. Inadaiwa kwamba wanatoa kisingizio cha UFISADI alioufanya Mkapa kwa kuuza kinyemela hisa za serikali katika Mobitel (sasa TIGO) na hivyo Tigo sasa inamilikiwa kwa asilimia 100 na wageni lakini sheria inakataza. Wanajaribu kutoa tafsiri ya kisheria kupotosha kwamba eti sheria ilikua na maana na kuanzishwa tu then baadaye mzalendo anaweza kuuza popote wakitoa mfano wa TIGO walkati TIGO ni UFISADI wa Mkapa na genge lake. Sasa Chenge (akiwa Miundombinu) aliandika waraka kwa AG Mwanyika akitoa maeleekezo ya kutaka RA aachiwe auze hisa zake. AG inasemekana alikataa kabla ya kubanwa na kulegeza kamba, na baaaye Bodi ya TCRA ikagawanyika kabla ya kupitisha lakini Management hadi sasa ina maoni tofauti kuhusu uamuzi wa bodi, Inasema sawa, bodi ina uamuzi lakini si kukiuka sheria, sasa kazi ipo maana wanaandaa mabadiliko ya Sheria Ndogo (regulation) ambayo zamani ilikua Waziri anaweza kubadili tu kwa kutangaza katika gazeti la serikali (GN) lakini sasa Samuel Sitta, anaelezwa kuwa kizingiti kwa kuunda kamati ya bunge ya Sheria Ndogo ambayo sasa italazmika kupitia kwanza sheria ndogo kabla haijatangazwa katika GN. Ndio maana kulikua na mkakati maalumu wa kumng'oa Sitta ili kuruhusu hiyo regulation tena inabadilishwa kwa sababu ya mtu mmoja tu, RA.

Hima mtanzania, tuwahawi mafisadi kabla hawajatuwahi. Sambaza ujumbe huu kwenye email za watanzania wengine mpaka kieleweke! Kwa maelezo zaidi wasiliana nami kupitia ashabdala@yahoo.com ama ashawazenj@gmail.com ama tembelea http://ashawazenj.blogspot.com

Kwa nguvu ya umma, tutawashinda mafisadi na kupata Tanzania yenye neema.

Asha Abdala

No comments: