Thursday 16 April 2009

The Articles of Union

THE ARTICLES OF UNION
between
THE REPUBLIC OF TANGANYIKA AND THE PEOPLES' REPUBLIC OF ZANZIBAR
WHEREAS the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples' Republic of Zanzibar being mindful of the long association of the peoples of these lands and of their ties of kinship and amity, and being desirous of furthering that associatio! n and strengthening of these ties and of furthering the unity of African peoples have met and considered the union of the Republic of Tanganyika with the Peoples Republic of Zanzibar:
AND WHEREAS the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples'Republic of Zanzibar are desirous that the two Republics shall be united in one Sovereign Republic in accordance with the Articles hereinafter contained:-
It is therefore AGREED between the Governments of the Republic of Tanganyika and of the Peoples' Republic of Zanzibar as follows: -
(i) The Republic of Tanganyika and the Peoples' Republic of Zanzibar shall be united in one Sovereign Republic.
(ii) During the period from the commencement of the union until the Constituent Assembly provided for in Article (vii) shall have met and adopted a Constitution for the united Republic (hereinafter referred to as the interim period) the united Republic
(i! ii) to (vi).
shall be governed in accordance with the provisions of Articles
(iii) During the interim period the Constitution of the united Republic shall be the Constitution of Tanganyika so modified as to provide for-
(a) a separate legislature and executive in and for Zanzibar from time to time constituted in accordance with the existing law of Zanzibar and having exclusive authority within Zanzibar for matters other than those reserved to the Parliament and Executive of the united Republic;
(b) the offices of two Vice-Presidents one of whom (being. a person normally resident in Zanzibar) shall be the head of the aforesaid executive in and for Zanzibar and shall be the principal assistant of the President of the United Republic in the discharge of his executive functions in relation to Zanzibar;
(c) the representation of Zanzibar in the Parliament of the United Republic;
(d) such other matters! as may be expedient or desirable to give effect to the united Republic and to these Articles.
(iv) There shall reserved to the Parliament and Executive of the united Republic the following matters-
(a) The Constitution and Government of the united Republic.
(b) External Affairs.
(c) Defence.
(d) Police.
(e) Emergency Powers.
(f) Citizenship.
(g) Immigration.
(h) External Trade and Borrowing.
(i) The Public Service of the united Republic.
(j) Income Tax, Corporation Tax, Customs and Excise.
(k) Harbours, Civil Aviation, Posts and Telegraphs.
And the said Parliament and Executive shall have exclusive authority in such matters throughout and for the purposes of the united Republic and in addition exclusive authority in respect of all other matters in and for Tanganyika.
(v) The existing laws of Tanganyika and of Zanzibar shall remain in force in their respective territories subject-
(a) to any provision made hereafter by a competent legislature;
(b) to such provision as may be made by order of the President of the united Republic for the extension to Zanzibar of any law relating to any of the matters set out in Article (iv), and the revocation of any corresponding law of Zanzibar;
(c) to such amendments as may be expedient or desirable to give effect to the union and to these Articles.
(v) (a) The first President of the united Republic shall be Mwalimu Julius K. Nyerere and he shall carry on the Government of the united Republic in accordance with the provisions of these Articles and with the assistance of the Vice-Presidents aforesaid and of such other ministers and officers as he may appoint from Tanganyika and Zanzibar and their respective public services.
(b) The first Vice-President from Zanzibar to be appointed in accordance with the modifications provid! ed for in Article (iii) shall be Sheikh Abeid Karume.
(vii) The President of the united Republic: in agreement with the Vice-President who is head of the Executive in Zanzibar shall-
(a) Appoint a Commission to make proposals for a Constitution for the united Republic.
(b) Summon a Constituent Assembly composed of Representatives from Tanganyika and from Zanzibar in such numbers as they may determine to meet within one year of the commencement of the union for the purpose of considering the proposals of the Commission aforesaid and to adopt a Constitution for the united Republic.
(viii) These Articles shall be subject to the enactment of laws by the Parliament of Tanganyika and by the Revolutionary Council of the Peoples' Republic of Zanzibar in conjunction with the Cabinet of Ministers thereof, ratifying the same and providing for the Government of the united Republic and of Zanzibar in accordance therewith.
IN WITNESS WHERE Julius K. Nyerere, the President of the Republic of Tanganyika, and Abeid Karume the President of the Peoples' Republic of Zanzibar have signed these Articles, in duplicate, at Zanzibar, on this twenty-second day of April, 1964.
Passed in the National Assembly on the twenty-fifth day of April, 1964.

Thursday 22 January 2009

Mambo ya UVCCM Zanzibar

Hivi ndivyo vijana wa CCM walivyoponda raha, Nami nilishuhudia


2009-01-22 10:32:47 Na Mwinyi Sadallah, Zanzibar
Kiwango cha fedha ambacho mkutano wa watu 100 wa siku nne wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) zilitafunwa kimegundulika, na sasa kimeacha maswali mengi juu ya matumizi makubwa kiasi hicho wakati umoja huo ukiwa hoi kimapato. Uchunguzi wa Nipashe kutoka vyanzo mbalimbali visiwani Zanzibar ulikofanyika mkutano huo vimesema kwamba kwa wastani matumzi hayo yalikuwa ni nusu bilioni ambazo zilijumuisha usafiri wa ndani, chakula na malazi katika hoteli ya kifahari ya Zamani Kempinski. Fedha hizo ambazo kwa viwango vyovyote ni nyingi kwa hali ya uchumi wa UVCCM ambayo ilisaidiwa fedha za kuendesha mkutano mkuu wa uchaguzi hivi karibuni na mfanyabishara mmoja, hakuna kiongozi yeyote wa umoja huo aliyekuwa tayari kueleza kwamba zilitoka wapi. Kwa wastani, kiasi hicho cha fedha kwa wajumbe 100 kikikokotolewa kila mjumbe atakuwa ametumia walau Shilingi milioni nne katika siku hizo sawa na Shilingi milioni moja kwa siku. Jambo ambalo linazidi kutia shaka na madai kuwa, malipo yote ya mkutano huo mkubwa uliohudhuriwa na Rais Mstaafu wa Afrika ya Kusini, Thabo Mbeki, yaliratibiwa na Januari Makamba ambaye ni msaidizi wa Rais Jakaya Kikwete anayeshughulikia hotuba na pia ni mtoto wa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. Hata hivyo, Januari alipotafutwa na Nipashe hakuwa tayari kueleza nafasi yake katika mkutano huo kwani si kiongozi ndani ya UVCCM. Taarifa zilizopatikana juzi zilisema gharama za huduma za malazi ziligawanyika katika makundi manne. Kundi la kwanza la kada ya chini katika chama lilikuwa likilipiwa huduma ya malazi Sh 466,200 kwa siku, kundi la pili lilikuwa likilipiwa Sh 574,200, kundi la tatu lilikuwa likilipiwa Sh 738,00 na kundi la nne lilikuwa likilipiwa Sh milioni 1.9. Uchunguzi wa Nipashe umebaini kwamba kiasi cha Sh milioni 200 kati ya fedha zote zilizotumika zimetolewa na mfanyabiashara mmoja (jina tunalo) na nyingine zilizobaki hazijulikani zilikopatikana. Uchunguzi wa Nipashe pia umebaini kwamba pamoja na UVCCM kutumia kiasi hicho kikubwa cha fedha, bado kuna baadhi ya vyumba vililipiwa bila ya wahusika kulala kati ya vyumba 114 walivyokodi kwa sababu wengine walikuwa wanakwenda na kuondoka kutokana na majukumu mengine waliyopangiwa. Imefahamika baadhi ya wajumbe walikuwa pia wakihudhuria mkutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Soko la Pamoja la Nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) uliofanyika Zanzibar Beach Resort iliyopo Mbweni, kiasi cha kilomita 47 kutoka hoteli ya Kempinski, mkutano wa UVCCM ulipofanyika. Wajumbe wengine walikodiwa katika hoteli ya ya Fairmont iliyopo Mkoa wa Kaskazini Unguja na kusababisha huduma za usafiri kwa wajumbe kufikia Sh milioni 6.4. Huduma za malazi zilifikia Sh milioni 216.4 kwa hoteli ya Kempinski peke yake mbali ya gharama nyingine zilizotumika kukodi hoteli ya Fairmont. Aidha, gharama za huduma za chakula kwa wajumbe zaidi ya 100 zilifikia Sh milioni 49.6.Huduma nyingine za kurudufu, uchapishaji na matumizi ya vifaa vya hoteli pia zilitumika. Viongozi wakongwe wa siasa waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Makamu Mwenyekiti wa CCM, (Tanzania Bara), Pius Msekwa, Kingunge Ngombare Mwiru, Mzee Hassan Nassor Moyo, Balozi Job Lusinde, Balozi Juma Mwapachu na Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa. Hata hivyo, Mwenyekiti wa Tiafa UVCCM, Hamad Masauni Yussuf, alipopigiwa simu na Nipashe kuzungumzia mkutano huo, alitoa udhuru kwamba asingeweza kuzungumza kwa kuwa alikuwa anahudhuria kikao. Habari kutoka katika kongamano la UVCCM limeeleza kuwa wajumbe wengi waliupongeza uongozi mpya kwa kufanikisha mkutano huo, baadhi ya wajumbe walifurahi kusafirishwa kwa ndege na kuwekwa katika hoteli ya hadhi ya kimataifa. ``Kwa kweli wajumbe wengi wanaupongeza uongozi mpya wa UVCCM kwa kuwahudumia katika hadhi ya kimataifa,`` alisema mjumbe mmoja mwenye cheo cha juu katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ). Alisema kitendo cha baadhi ya wajumbe kusafirishwa kwa ndege kilichukua nafasi kubwa kwa kutolewa shukrani katika kikao hicho. Mkutano huo umezua mjadala mkali baadhi ya wajumbe wakisema hakukuwa na haja ya mkutano huo kufanyika katika hoteli ya bei kubwa wakati CCM inazo kumbi kadhaa za mikutano kwa mfano ukumbi wa CCM Kisiwandui. Aidha, ilielezwa kuwa Hoteli ya Bwawani ambapo chumba ni Sh 50,000 kwa siku ingelitumika kwa mkutano huo na fedha zingebaki kusaidia mambo mengine ya kuimarisha chama. Gazeti hili lilipowasiliana na Katibu Mkuu wa UVCCM, Isack Francis, alisema hakuna haja ya kuhoji matumizi ya fedha hizo, kwa vile Nipashe haikushiriki kutoa mchango. ``Ninyi mnahoji nini, kwani fedha hizo mlichanga nyie, hili ni suala letu tuachieni wenyewe, hatujawahi kuwaomba hela yoyote, haya matumizi hayawahusu,`` alisema kwa kuhamaki. Francis alisema uamuzi wowote uliohusu kongamano hilo, ikiwemo uteuzi wa hoteli ya kitalii ya Zamani Kempinski ya visiwani Zanzibar, unaihusu UVCCM. ``UVCCM ni taasisi kubwa, ina vyanzo vingi vya fedha, hata hiyo hoteli ya kitalii tuliamua kuitumia kama wanavyoamua watu wengine, hivyo haiwahusu,`` alisema na kukata simu. Kwa upande wake, Januari Makamba, alisema ushiriki wake katika kongamano hilo, ulitokana na mwaliko ambao hata hivyo, hakusema ulitolewa na nani. Makamba aliyesisitiza kutopenda kuzungumza na vyombo vya habari, alisema akiwa katika kongamano hilo, alishiriki kumsaidia Mwenyekiti wa UVCCM, kutekeleza baadhi ya kazi za kongamano hilo. Hata hivyo, alipoulizwa kuzitaja kazi hizo, Makamba, alikataa na kusema suala hilo linapaswa kutolewa ufafanuzi na UVCCM. Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, John Chiligati, alisema sakata la matumizi ya fedha hizo,linapaswa kutolewa ufafanuzi na UVCCM wenyewe. Alisema Umoja huo ni kama mtoto aliyefikia hatua ya kujitenga katika familia, hivyo kuendesha mambo yake kwa kadri alivyojipangia. ``Hawa UVCCM wanajitegemea kwa vyanzo vya fedha na hata kanuni za matumizi yake...hilo ni swali zuri, watafute wenyewe watoe ufafanuzi,`` alisema.
SOURCE: Nipashe

Friday 20 June 2008

Rostam Aziz na Vodacom-Tususie Ufisadi

Rostam Aziz yule mtanzania mwenye asili ya Kiiran aliyeko kwenye Orodha ya Mafisadi(List of Shame) anamiliki zaidi ya asilimia 30 ya hisa za Kampuni ya Simu za Mkononi ya Vodacom kupitia kwa Kampuni yake ya Caspian ambayo pia inahusika na ufisadi katika kandarasi mbalimbali za ujenzi wa barabara, viwanja na hata migodoni. Je, wewe ni mtanzania unayechukia ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka?


Andika ujumbe huu na mtumie mwenzako mwenye Vodacom kwa SMS:

“Imegundulika, mtaji wa Vodacom sehemu kubwa ni fedha za ufisadi toka kwa Rostam Aziz. Tumia mtandao mwingine kuepuka kulipa fedha zako kuendeleza ufisadi. Ukijitoa kwenye ufisadi, unawapunguzia nguvu mafisadi. Sambaza Ujumbe”Au tuma ujumbe huu:“Afrika Kusini walivunja nguvu ya makuburu. Acha kuendelea kutunisha faida ya Fisadi Rostam Aziz. Achana na kampuni yake ya Vodacom. Tumia mtandao mwingine”.Au:“Je, wajua? Rostam Aziz anahisa nyingi Vodacom kwa fedha za ufisadi. Je, unataka kumwongezea fedha zaidi za kufanya ufisadi nchini? Okoa Taifa, jiunge na simu nyingine”.Au:“Kwanini utende dhambi kwa kuchangia katika ufisadi? Rostam Aziz ni mmoja wa wamiliki wa Vodacom. Tafakari, Chukua hatua”Au:“Ukipiga simu ana kutuma ujumbe kwa kutumia Vodacom unawaneemesha wamiliki mafisadi wakina Rostam Aziz, Noni na makuburu wa Afrika Kusini. Chagua ni lako”Au:“Vodacom, muondoe Rostam Aziz kabla watanzania hatujaucha mtandao wenu kwa kumilikiwa na watuhumiwa wa ufisadi. Tuma ujumbe huu kwenda 123, na mtumie na mwenzio”Au“Ama piga simu huduma kwa wateja namba 100; waulize Vodacom, je Rostam Aziz ni mmoja wa wamiliki? Wanasubiri nini mkutoa kwa ufisadi wake?
Habari za uhakikia kabisa ni kwamba Rostam Aziz ameanza kuhamishia mali zake nje ya nchi, sababu anahofia mambo yanavyokwenda serikalini kwa sasa. Kwa ushahidi tayari ameweka rehani hisa zake zote 35pc za Vodacom Afrika Kusini. Kabla ya kuhamishia hisa zake, alikua amenunua hisa za Planetel za mwenzake Peter Noni na mkewe, naye alifanya hivyo kuhofia mambo yanavyokwenda ofisini kwake BoT. Rostam alichukua hisa zote 35pc za Watanzania kupitia kampuni zake za Caspian na Mirambo. Chenge akiwa Waziri wa miundombinu alimsaidia kwa nguvu zake zote Rostam kufanikisha mkakati wake huo wa kuhamisha hisa zake nje kwa kisingizio cha kuweka rehani. Kuna watu serikalini walipinga (na wanaendelea kupinga) lakini jamaa aliwazidi kete kwa kusadiwa na Chenge na sasa inaelekea amefanikiwa kwa kiasi.

Sheria ya TCRA inasema kuhusu hisa za wazalendo kwamba wageni wasimiliki hisa zaidi ya 65% lakini Rostam Aziz aka RA anataka kuzipeleka nje zote. Inadaiwa kwamba wanatoa kisingizio cha UFISADI alioufanya Mkapa kwa kuuza kinyemela hisa za serikali katika Mobitel (sasa TIGO) na hivyo Tigo sasa inamilikiwa kwa asilimia 100 na wageni lakini sheria inakataza. Wanajaribu kutoa tafsiri ya kisheria kupotosha kwamba eti sheria ilikua na maana na kuanzishwa tu then baadaye mzalendo anaweza kuuza popote wakitoa mfano wa TIGO walkati TIGO ni UFISADI wa Mkapa na genge lake. Sasa Chenge (akiwa Miundombinu) aliandika waraka kwa AG Mwanyika akitoa maeleekezo ya kutaka RA aachiwe auze hisa zake. AG inasemekana alikataa kabla ya kubanwa na kulegeza kamba, na baaaye Bodi ya TCRA ikagawanyika kabla ya kupitisha lakini Management hadi sasa ina maoni tofauti kuhusu uamuzi wa bodi, Inasema sawa, bodi ina uamuzi lakini si kukiuka sheria, sasa kazi ipo maana wanaandaa mabadiliko ya Sheria Ndogo (regulation) ambayo zamani ilikua Waziri anaweza kubadili tu kwa kutangaza katika gazeti la serikali (GN) lakini sasa Samuel Sitta, anaelezwa kuwa kizingiti kwa kuunda kamati ya bunge ya Sheria Ndogo ambayo sasa italazmika kupitia kwanza sheria ndogo kabla haijatangazwa katika GN. Ndio maana kulikua na mkakati maalumu wa kumng'oa Sitta ili kuruhusu hiyo regulation tena inabadilishwa kwa sababu ya mtu mmoja tu, RA.

Hima mtanzania, tuwahawi mafisadi kabla hawajatuwahi. Sambaza ujumbe huu kwenye email za watanzania wengine mpaka kieleweke! Kwa maelezo zaidi wasiliana nami kupitia ashabdala@yahoo.com ama ashawazenj@gmail.com ama tembelea http://ashawazenj.blogspot.com

Kwa nguvu ya umma, tutawashinda mafisadi na kupata Tanzania yenye neema.

Asha Abdala

Monday 9 June 2008

Suluhisho la Zanzibar

na Mwandishi Wetu
WAKATI harakati za kuyafufua mazungumzo ya kusaka suluhu ya mpasuko wa kisiasa visiwani Zanzibar zikionekana kushindwa, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kina dawa ya kudumu ya mpasuko huo.
Akizungumza na Tanzania Daima mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema mfumo wa majimbo, ambao umeasisiwa na chama hicho, unaweza kuwa suluhu ya matatizo ya kisiasa yanayoikabili Zanzibar hivi sasa.
Mbowe alisema kuwa kitu kikubwa kinachoumiza vichwa kuhusu masuala ya Zanzibar, ni mfumo unaofaa kwa utawala, kutokana na hali halisi kuonyesha kutoshana nguvu kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF).
Alisema CUF imeshaonyesha dhahiri kuwa imekikamata Kisiwa cha Pemba, na kwamba hakuna linaloweza kufanyika hivi sasa kidemokrasia kuzuia nguvu za chama hicho kisiwani humo.
“Kinachotakiwa ni kuwaachia CUF waunde serikali yao huko Pemba na chini ya sera yetu ya majimbo jambo hili linawezekana… tunacholenga katika sera hii ni kuwapa watu uwezo na haki ya kujitawala wenyewe, kuamua aina ya viongozi wanaowataka na kujipangia masuala yao wenyewe bila kuingiliwa na serikali kuu,” alisema.
Mbowe alibainisha kuwa, iwapo hilo litafanyika kwa kuanzisha Jimbo la Pemba, CUF wanaweza kuendesha serikali ya jimbo hilo, kama ambavyo vyama vingine vinaweza kuendesha serikali za majimbo watakakoshinda.
Akifafanua, Mbowe alisema kuwa ingawa wapo baadhi ya watu wanaiona sera hiyo kuwa inaweza kusababisha mgawanyiko, lakini iwapo itafuatwa kwa mujibu wa kanuni na taratibu, itasaidia zaidi kuwaunganisha Watanzania.
“Mfumo huu utawapa haki na uhuru zaidi watu wa kujipangia mambo yao, hivyo utawafanya wajione huru zaidi,” alisema na kubainisha kuwa katika mazingira kama hayo, manung’uniko yanayoweza kusababisha chuki miongoni mwa wananchi, yatapungua.
Alisema kuwa dhima kuu ya sera hiyo imegawanyika katika sehemu kadhaa, ikiwamo kurekebisha mfumo wa utawala na kuwawezesha wananchi wa eneo husika kuwachagua viongozi wao wenyewe moja kwa moja.
Alisema mfumo wa sasa ambao baadhi ya viongozi wanateuliwa kama vile wakuu wa mikoa na wilaya, unawafanya washindwe kuwatumikia watu ipasavyo, kwani uwajibikaji wao huwa katika mamlaka iliyowateua na si watu wanaowaongoza.
“Ndio maana tuna wakuu wa mikoa ambao wananchi wengi katika mikoa wanayoiongoza hawawafahamu… wanateuliwa kwa utashi wa mtu mmoja tu na hii ni hatari. Tunachotaka sisi kupitia sera hii ni watu kuchagua viongozi wao katika jimbo lao kutokana na jinsi ambavyo wanawafahamu,” alisema.
Pia, alisema sera hiyo inatasaidia kusisimua uchumi, kwani inalenga kuyafanya maeneo tofauti yashindane kiuchumi.
Mbowe, alisema kila jimbo litakuwa na wajibu wa kukusanya mapato yake, na kuyapangia bajeti ya matumizi, huku likiwajibika kutoa mchango wake kwa Serikali Kuu, kutokana na uwezo wake wa kukusanya mapato.
Alisema Serikali Kuu itaachiwa majukumu manne makubwa na aliyataja kuwa ni uhamiaji, masuala ya ulinzi na usalama, mambo ya nje na masuala ya sarafu na sera za fedha.
“Mtindo wa sasa wa kukusanya mapato yote na kuyaweka kwenye kapu moja (hazina) ni mbaya kwa sababu unawafanya watu wanaodhibiti hiyo hazina wajione kuwa wana fedha, nyingi hivyo kuzitumia hovyo,” alisema.

Sera ya Majimbo Suluhu ya Kisiasa Zanzibar?

CHADEMA: Tuna dawa ya mpasuko Zanzibar
na Mwandishi Wetu
WAKATI harakati za kuyafufua mazungumzo ya kusaka suluhu ya mpasuko wa kisiasa visiwani Zanzibar zikionekana kushindwa, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kina dawa ya kudumu ya mpasuko huo.
Akizungumza na Tanzania Daima mwishoni mwa wiki, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema mfumo wa majimbo, ambao umeasisiwa na chama hicho, unaweza kuwa suluhu ya matatizo ya kisiasa yanayoikabili Zanzibar hivi sasa.
Mbowe alisema kuwa kitu kikubwa kinachoumiza vichwa kuhusu masuala ya Zanzibar, ni mfumo unaofaa kwa utawala, kutokana na hali halisi kuonyesha kutoshana nguvu kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF).
Alisema CUF imeshaonyesha dhahiri kuwa imekikamata Kisiwa cha Pemba, na kwamba hakuna linaloweza kufanyika hivi sasa kidemokrasia kuzuia nguvu za chama hicho kisiwani humo.
“Kinachotakiwa ni kuwaachia CUF waunde serikali yao huko Pemba na chini ya sera yetu ya majimbo jambo hili linawezekana… tunacholenga katika sera hii ni kuwapa watu uwezo na haki ya kujitawala wenyewe, kuamua aina ya viongozi wanaowataka na kujipangia masuala yao wenyewe bila kuingiliwa na serikali kuu,” alisema.
Mbowe alibainisha kuwa, iwapo hilo litafanyika kwa kuanzisha Jimbo la Pemba, CUF wanaweza kuendesha serikali ya jimbo hilo, kama ambavyo vyama vingine vinaweza kuendesha serikali za majimbo watakakoshinda.
Akifafanua, Mbowe alisema kuwa ingawa wapo baadhi ya watu wanaiona sera hiyo kuwa inaweza kusababisha mgawanyiko, lakini iwapo itafuatwa kwa mujibu wa kanuni na taratibu, itasaidia zaidi kuwaunganisha Watanzania.
“Mfumo huu utawapa haki na uhuru zaidi watu wa kujipangia mambo yao, hivyo utawafanya wajione huru zaidi,” alisema na kubainisha kuwa katika mazingira kama hayo, manung’uniko yanayoweza kusababisha chuki miongoni mwa wananchi, yatapungua.
Alisema kuwa dhima kuu ya sera hiyo imegawanyika katika sehemu kadhaa, ikiwamo kurekebisha mfumo wa utawala na kuwawezesha wananchi wa eneo husika kuwachagua viongozi wao wenyewe moja kwa moja.
Alisema mfumo wa sasa ambao baadhi ya viongozi wanateuliwa kama vile wakuu wa mikoa na wilaya, unawafanya washindwe kuwatumikia watu ipasavyo, kwani uwajibikaji wao huwa katika mamlaka iliyowateua na si watu wanaowaongoza.
“Ndio maana tuna wakuu wa mikoa ambao wananchi wengi katika mikoa wanayoiongoza hawawafahamu… wanateuliwa kwa utashi wa mtu mmoja tu na hii ni hatari. Tunachotaka sisi kupitia sera hii ni watu kuchagua viongozi wao katika jimbo lao kutokana na jinsi ambavyo wanawafahamu,” alisema.
Pia, alisema sera hiyo inatasaidia kusisimua uchumi, kwani inalenga kuyafanya maeneo tofauti yashindane kiuchumi.
Mbowe, alisema kila jimbo litakuwa na wajibu wa kukusanya mapato yake, na kuyapangia bajeti ya matumizi, huku likiwajibika kutoa mchango wake kwa Serikali Kuu, kutokana na uwezo wake wa kukusanya mapato.
Alisema Serikali Kuu itaachiwa majukumu manne makubwa na aliyataja kuwa ni uhamiaji, masuala ya ulinzi na usalama, mambo ya nje na masuala ya sarafu na sera za fedha.
“Mtindo wa sasa wa kukusanya mapato yote na kuyaweka kwenye kapu moja (hazina) ni mbaya kwa sababu unawafanya watu wanaodhibiti hiyo hazina wajione kuwa wana fedha, nyingi hivyo kuzitumia hovyo,” alisema.

Tuesday 29 April 2008

Wasomi waukosoa Muungano

Wasomi waukosoa Muungano
na Mwanne Mashugu, Zanzibar
SIKU moja baada ya kupita kwa sherehe za miaka 44 ya Muungano, wanafunzi kadhaa wa vyuo vikuu visiwani hapa, wamesema mabadiliko kuhusu hadhi ya Rais wa Zanzibar katika Serikali ya Muungano, ni kasoro kubwa inayopaswa kurekebishwa haraka.
Kutokana na kasoro hiyo, wanafunzi hao walishauri Serikali ya Muungano kurejesha haraka utaratibu wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Walisema marekebisho ya sheria yaliyomuondolea hadhi Rais wa Zanzibar kushika wadhifa huo, umeishushia hadhi yake Zanzibar katika nyanya ya kimataifa.
Wanafunzi hao walisema hayo walipokuwa katika kongamano kuadhimisha miaka 44 ya Muungano wa Tanzania.
Hadhi ya Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Muungano iliondolewa kupitia mabadiliko ya 11 ya Katiba ya Muungano.
“Rais wa Zanzibar mamlaka yake yameondoka katika nyanja za kimataifa na uraia wetu umepotea kwa vile hata misaada inaishia Tanzania Bara,” alisema Khamis Issa Mohammed wa Chuo cha Elimu Chukwani.
Katika kongamano hilo lililoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, Haji Habib Kombo alisema kwamba hivi sasa Rais wa Zanzibar analazimika kuingia katika Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano kama waziri asiyekuwa na wizara maalum, jambo ambalo halileti picha nzuri.
Aidha, mwanafunzi huyo alibainisha kuwa hata mfumo uliopo, hauonyeshi kinagaubaga mamlaka aliyonayo makamu wa rais.
Akifafanua, alisema kuwa licha ya taratibu kueleza vinginevyo, lakini hali halisi inaonyesha kuwa mamlaka ya utendaji ya Waziri Mkuu ni makubwa kuliko ya Makamu wa Rais, suala ambalo linahitaji kuangaliwa upya, ili kurejesha hadhi ya Makamu wa Rais.
“Bila ya Zanzibar hakuna Tanzania, na bila ya Afro Shiraz Party hakuna CCM… marekebisho ya katiba yafanyike kumpa hadhi Rais wa Zanzibar,” alisisitiza.
Alieleza kuwa mfumo huo mbaya wa Muungano, hauathiri katika masuala ya utawala pekee, bali pia katika nyanja nyingine.
Alisema kuwa kutokana na mfumo huo, Zanzibar imekuwa ikiathirika kiuchumi na kutoa mfano kuwa pamoja na elimu ya juu kuwa suala la Muungano, hakuna chuo kikuu hata kimoja kilichojengwa na Serikali ya Muungano visiwani Zanzibar.
Kombo alisema kwamba Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kinapaswa kupokea ruzuku kutoka Serikali ya Muungano, badala ya kuendeshwa kwa gharama za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar peke yake kama ilivyo sasa.
Issa Kheri wa Chuo cha Elimu Chukwani alisema kwamba kero za Muungano zinachelewa kupatiwa ufumbuzi kutokana na viongozi kutozipa umuhimu.
Alisema kwamba zipo ripoti nyingi zilizokusanywa juu ya Muungano, ikiwemo ile ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, lakini inashangaza kuwa hadi sasa mapendekezo yake hayajatekelezwa.
Alisema kwamba iwapo ripoti ya Jaji Kisanga na Francis Nyalali zingefanyiwa kazi, hivi sasa kero nyingi za Muungano zingekuwa zimeshamalizwa.
Alieleza kuwa badala ya kutekeleaa mapendekezo ya Tume ya Jaji Kisanga, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, alitumia muda mwingi kumshambulia jaji huyo, kwa kutoa ripoti hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inawakilisha maoni ya wananchi.
“Tume nyingi zimeundwa ikiwemo ile ya Jaji Kisanga, ikafanya kazi nzuri tu, lakini Rais mstaafu Mkapa akamshambulia kutokana na maoni yaliyopendekezwa na wananchi,” alisema.
Alieleza kwamba hakuna njia itakayosaidia kuwa na Muungano bora zaidi ya wananchi kushirikishwa na kuamua kwa kupitia utaratibu wa kura ya maoni.
Alisema kwamba hivi sasa historia ya Tanganyika ipo hatarini kupotea, kwa vile baadhi ya Watanzania wanaoishi Zanzibar wanapoambiwa wanatoka Tanganyika, wanahisi kama wanatukanwa.
Naye Omar Suleiman, alisema kwamba kero za Muungano haziwezi kutatuliwa kwa makongamano, bali kwa wananchi wa Zanzibar kujenga umoja, ili kuhakikisha matatizo yote ya Muungano yanatatuliwa kwa muda muafaka.
Alisema kwamba Zanzibar inashindwa kusonga mbele kutokana na tabia iliyojitokeza ya majungu na kuendeleza tofauti za Unguja na Pemba na hivyo kuzorotesha maendeleo ya wananchi.
“Jambo la msingi sisi Wazanzibari tuwe na msimamo, tuache tabia ya fitina na ubaguzi kwa misingi ya Upemba na Uunguja, ili tuweze kusonga mbele kutatua matatizo ya Muungano,” alisema.
Alisema Zanzibar hivi sasa ni nchi kamili yenye utawala wake, lakini rais wake hana nguvu nje ya Zanzibar.
Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Said Mzee, alisema kwamba Zanzibar inarudi nyuma kutokana na wasomi wake kuwa waoga na kushindwa kujitokeza kudai mambo ya msingi ya nchi yao.
Alisema kwamba njia nyingi za kiuchumi Zanzibar zimevurugwa na mfumo mbaya wa Muungano, lakini wasomi wengi wamekaa kimya licha ya wao na jamii kuguswa na masuala hayo.
Makamu mwenyekiti huyo alisema vikao vya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi havitasaida kutatua kero za Muungano. Alishauri kuwa watu wengi zaidi washirikishwe katika kujadili masuala ya Muungano, kwa vile mambo hayo yanagusa taifa na si CCM au serikali pekee.
Aidha, alisema kuwa udhaifu wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika utekelezaji majukumu yao, umechangia Zanzibar kukabiliwa na matatizo mengi ya kiuchumi yakiwemo yaliyo nje ya Muungano.
“Wawakilishi wetu hawana elimu ya kutosha katika kujadili mipango ya maendeleo na kiuchumi, ndiyo maana Baraza la Wawakilishi limedorora, hawa ni wazee wetu tunawaheshimu, lakini ukweli wanaburuzwa na serikali,” alisema.
Alieleza kwamba umefika wakati wajumbe wa baraza hilo kufuata nyayo za Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe, aliyekubali kujitolea kutetea maslahi ya wananchi na taifa.

Wasomi waukosoa Muungano

na Mwanne Mashugu, ZanzibarSIKU moja baada ya kupita kwa sherehe za miaka 44 ya Muungano, wanafunzi kadhaa wa vyuo vikuu visiwani hapa, wamesema mabadiliko kuhusu hadhi ya Rais wa Zanzibar katika Serikali ya Muungano, ni kasoro kubwa inayopaswa kurekebishwa haraka. Kutokana na kasoro hiyo, wanafunzi hao walishauri Serikali ya Muungano kurejesha haraka utaratibu wa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano. Walisema marekebisho ya sheria yaliyomuondolea hadhi Rais wa Zanzibar kushika wadhifa huo, umeishushia hadhi yake Zanzibar katika nyanya ya kimataifa. Wanafunzi hao walisema hayo walipokuwa katika kongamano kuadhimisha miaka 44 ya Muungano wa Tanzania. Hadhi ya Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Muungano iliondolewa kupitia mabadiliko ya 11 ya Katiba ya Muungano. “Rais wa Zanzibar mamlaka yake yameondoka katika nyanja za kimataifa na uraia wetu umepotea kwa vile hata misaada inaishia Tanzania Bara,” alisema Khamis Issa Mohammed wa Chuo cha Elimu Chukwani. Katika kongamano hilo lililoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Zanzibar Tunguu, Haji Habib Kombo alisema kwamba hivi sasa Rais wa Zanzibar analazimika kuingia katika Baraza la Mawaziri la Jamhuri ya Muungano kama waziri asiyekuwa na wizara maalum, jambo ambalo halileti picha nzuri. Aidha, mwanafunzi huyo alibainisha kuwa hata mfumo uliopo, hauonyeshi kinagaubaga mamlaka aliyonayo makamu wa rais. Akifafanua, alisema kuwa licha ya taratibu kueleza vinginevyo, lakini hali halisi inaonyesha kuwa mamlaka ya utendaji ya Waziri Mkuu ni makubwa kuliko ya Makamu wa Rais, suala ambalo linahitaji kuangaliwa upya, ili kurejesha hadhi ya Makamu wa Rais. “Bila ya Zanzibar hakuna Tanzania, na bila ya Afro Shiraz Party hakuna CCM… marekebisho ya katiba yafanyike kumpa hadhi Rais wa Zanzibar,” alisisitiza. Alieleza kuwa mfumo huo mbaya wa Muungano, hauathiri katika masuala ya utawala pekee, bali pia katika nyanja nyingine. Alisema kuwa kutokana na mfumo huo, Zanzibar imekuwa ikiathirika kiuchumi na kutoa mfano kuwa pamoja na elimu ya juu kuwa suala la Muungano, hakuna chuo kikuu hata kimoja kilichojengwa na Serikali ya Muungano visiwani Zanzibar. Kombo alisema kwamba Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar (SUZA) kinapaswa kupokea ruzuku kutoka Serikali ya Muungano, badala ya kuendeshwa kwa gharama za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar peke yake kama ilivyo sasa. Issa Kheri wa Chuo cha Elimu Chukwani alisema kwamba kero za Muungano zinachelewa kupatiwa ufumbuzi kutokana na viongozi kutozipa umuhimu. Alisema kwamba zipo ripoti nyingi zilizokusanywa juu ya Muungano, ikiwemo ile ya Tume ya Jaji Robert Kisanga, lakini inashangaza kuwa hadi sasa mapendekezo yake hayajatekelezwa. Alisema kwamba iwapo ripoti ya Jaji Kisanga na Francis Nyalali zingefanyiwa kazi, hivi sasa kero nyingi za Muungano zingekuwa zimeshamalizwa. Alieleza kuwa badala ya kutekeleaa mapendekezo ya Tume ya Jaji Kisanga, Rais wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa, alitumia muda mwingi kumshambulia jaji huyo, kwa kutoa ripoti hiyo ambayo kimsingi ilikuwa inawakilisha maoni ya wananchi. “Tume nyingi zimeundwa ikiwemo ile ya Jaji Kisanga, ikafanya kazi nzuri tu, lakini Rais mstaafu Mkapa akamshambulia kutokana na maoni yaliyopendekezwa na wananchi,” alisema. Alieleza kwamba hakuna njia itakayosaidia kuwa na Muungano bora zaidi ya wananchi kushirikishwa na kuamua kwa kupitia utaratibu wa kura ya maoni. Alisema kwamba hivi sasa historia ya Tanganyika ipo hatarini kupotea, kwa vile baadhi ya Watanzania wanaoishi Zanzibar wanapoambiwa wanatoka Tanganyika, wanahisi kama wanatukanwa. Naye Omar Suleiman, alisema kwamba kero za Muungano haziwezi kutatuliwa kwa makongamano, bali kwa wananchi wa Zanzibar kujenga umoja, ili kuhakikisha matatizo yote ya Muungano yanatatuliwa kwa muda muafaka. Alisema kwamba Zanzibar inashindwa kusonga mbele kutokana na tabia iliyojitokeza ya majungu na kuendeleza tofauti za Unguja na Pemba na hivyo kuzorotesha maendeleo ya wananchi. “Jambo la msingi sisi Wazanzibari tuwe na msimamo, tuache tabia ya fitina na ubaguzi kwa misingi ya Upemba na Uunguja, ili tuweze kusonga mbele kutatua matatizo ya Muungano,” alisema. Alisema Zanzibar hivi sasa ni nchi kamili yenye utawala wake, lakini rais wake hana nguvu nje ya Zanzibar. Akifungua kongamano hilo, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, Said Mzee, alisema kwamba Zanzibar inarudi nyuma kutokana na wasomi wake kuwa waoga na kushindwa kujitokeza kudai mambo ya msingi ya nchi yao. Alisema kwamba njia nyingi za kiuchumi Zanzibar zimevurugwa na mfumo mbaya wa Muungano, lakini wasomi wengi wamekaa kimya licha ya wao na jamii kuguswa na masuala hayo. Makamu mwenyekiti huyo alisema vikao vya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi havitasaida kutatua kero za Muungano. Alishauri kuwa watu wengi zaidi washirikishwe katika kujadili masuala ya Muungano, kwa vile mambo hayo yanagusa taifa na si CCM au serikali pekee. Aidha, alisema kuwa udhaifu wa wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar katika utekelezaji majukumu yao, umechangia Zanzibar kukabiliwa na matatizo mengi ya kiuchumi yakiwemo yaliyo nje ya Muungano. “Wawakilishi wetu hawana elimu ya kutosha katika kujadili mipango ya maendeleo na kiuchumi, ndiyo maana Baraza la Wawakilishi limedorora, hawa ni wazee wetu tunawaheshimu, lakini ukweli wanaburuzwa na serikali,” alisema. Alieleza kwamba umefika wakati wajumbe wa baraza hilo kufuata nyayo za Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe, aliyekubali kujitolea kutetea maslahi ya wananchi na taifa.